Ndoa na Familia

Utangulizi


Ndoa ilianzishwa na Mungu katika Edeni na ikathibitishwa na Yesu kuwa muungano wa maisha yote kati mwanaume na mwanamke katika wenzi wa upendo. Kwa Mkristo kifungo cha ndoa ni kwa Mungu na pia kwa mwenzi, na wenzi wanaokishiriki sharti wawe wenye imani moja tu. Upendo wa hiari, heshima staha na wajibu ndiso nyuzi za uhusiano huu, ambao utaakisi upendo, utakatifu, ukaribu kudumu kwa uhusiano kati ya Kristo na Kanisa lake. Kuhusu talaka, Yesu alifundisha kwamba mtu amwachaye mwenzi wake isipokuwa kwa sababu ya uasherati, na kuoa au kuolewa na mwingine azini. Ingawa uhusiano wa baadhi ya familia fulani huenda ukashindwa kufikia lengo, wenzi wa ndoa ambao hujitoa kamili kila mmoja kwa mwenzake katika Kristo wanaweza kufikia umoja wa upendo kupitia uongozi wa Roho na malezi ya kanisa. Mungu hubariki familia na anakusudia kwamba jamaa katika familia watasaidiana wao kwa wao kufkia upevu kamili. Wazazi wawalee watoto wao kumpenda na kumtii BWANA. Kwa kielelezo chao na maneno yao wawafundishe kwamba Kristo ni mtiishaji mwenye upendo, daima mpole na mwenye kujali, ambaye anawataka wawe viungo vya mwili wake, familia ya Mungu. Kukuza uhusiano wa karibu katika familia ni mojawapo ya alama ya kujulisha ujumbe wa injili ya mwisho. (Mwa.2:18-25; Yoh.2:1-22; 2Kor.6:14; Efe.5:21-33; Mt.5:31, 32; Mk. 10:11, 12; Luk.16:18; 1Kor.7:10, 11; Kut.20:12; Efe.6:1-4; Kumb.6: 5-9; Mith. 22:6; Mal. 4: 5, 6)

Nyumbani ni mahali pa msingi pa kurejeza sura ya Mungu kwa wanaume na wanawake. Katika familia, baba, mama na watoto wanaweza kujieleza kikamilifu, wakitimiza mahitaji yao ya kuhusiana, kupendana na kuthaminiana. Nyumba pia ni mahali ambako neema ya Mungu, ile misingi ya kikristo inapofanyiwa mazoezi na thamani zake zikamishwa kutoka kizazi kimoja kwenda kingine. Nyumbani ni mahali pa furaha kubwa. Vile vile nyumbani panaweza pakawa mahali pa maumivu makali. Maisha ya maelewano hudhihirisha misingi ya kikristo na kufunua tabia ya Mungu. Bahati mbaya maisha ya namna hii ni magumu kupatikana kwenye nyumba nyingi. Badala yake kinachoonekana, ni maisha yenye kufunua mioyo ya kibinadamu iliyojaa ubinafsi – magomvi, uasi, ushindani, hasira, ubaya na hata ukatili. Haya hayakuwa sehemu ya mpango wa awali wa Mungu tangu awali. Yesu alisema, “tangu mwanzo haikuwa hivi.” (Mt.19:8)

Tangu Mwanzo

Sabato na ndoa ni karama mbili za asili za Mungu kwa mwanadamu. Zilikusudiwa kumfurahisha mwanadamu kwa kumpa mwanadamu pumziko na kuthaminiana. Vilikuwa ni viwili vilivyokamilisha kazi ya Mungu ya uumbaji na kuufanya uwe mwema sana. (Mwa.1:31). Kwa kuanzisha sabato, Mungu alimpa mwanadamu wakati wa kupumzika na kufanywa upya, wakati wa ushirika naye. Kwa kuunda familia ya kwanza, Mungu aliunda msingi wa kijamii, kuwapa ufahamu wa kuthaminiana na fursa ya kufanya huduma kwa Mungu na kwa wanadamu.

Mwanamume na Mwanamke kwa Mfano wa Mungu.

Mwanzo 1:26, 27 inasimulia uumbaji wa Mungu ambao ungekalia dunia. “Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale … Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba mwanamume na mwanamke.” Siyo kwamba neno mtu linamaanisha mwanamume aliumbwa kwa sura ya Mungu, halafu Mwanamke akaumbwa kwa mfano wa mwanamume bali wote mwanaume na mwanamke waliumbwa kwa mfano na sura ya Mungu. Kama ambavyo Baba, Mwana na Roho Mtakatifu ni Mungu, mwanamume na mwanamke ndio wanaofanya mtu. Kama Mungu, bado ni wamoja kwa asili, kwa tathmini, lakini siyo nafsi moja. (cf. Yoh.10:30; 1Kor. 11:3). Maumbile yao hujaliza upungufu wa upande mwingine na utendaji wake ni wa kushirikiana.

Jinsia zote mbili ni njema (Mwa.1:31) pamoja na majukumu yake kutofautiana. Familia na nyumba hujengwa kwa utofauti wa jinsia. Mungu angeweza kufanyiza namna tofauti ya kuzaana kama ilivyo kwa viumbe wengine. Ulimwengu wa jinsia moja peke yake hautakuwa mkamilifu. Kuridhika kwa kweli kunawezekana tu katika jamii ambayo inahusisha wa kiume na wa kike. Usawa siyo suala la kuuliza hapa kwa sababu jinsia zote ni muhimu.

Katika siku yake ya kwanza, Adamu, mzaliwa wa kwanza na hivyo kiongozi wa wanadamu wote, alijisikia tofauti, hapakuwa na wa kufanana naye (Mwa.2:20). Mungu aliliona hitaji hili na ndiyo maana akasema siyo vema mtu huyu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye. (Mwa.2:18). Neno neged lililotumika hapa, lina maana ya kusimama kando au mbele ya, kuwa kinyume cha, kushabihiana ya moja au kitu. Kwa hiyo Mungu alimletea Adamu usingizi mzito, na akitumia ubavu wake moja, (Mwa.2:21, 22), alimtengenezea Adamu mwenzi wake. Alipozinduka kutoka usingizi wake, Adam mara moja alitambua uhusiano wa karibu ambao kitendo maalum cha uumbaji kimewezesha. Alisema kwa mshangao “sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume. (Mwa.2:23 cf. 1Kor.11:8).

Ndoa.

Kutoka kwenye tofauti ya wanaume na wanawake, Mungu alileta utaratibu – umoja. Ijumaa ya kwanza, aliunda ndoa ya kwanza akiwaunganisha wawili kuwa moja. Na ndoa imekuwa msingi wa familia, msingi wa jamii tangu wakati huo. Biblia huizungumzia ndoa kuwa inatokana na uamuzi wa vipande viwili kuunganishwa na kuwa kitu kimoja. Mmoja “atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili moja.” (Mwa.2:24).

1. Kuacha.

Msingi muhimu kwa ndoa ni kuachana na mahusiano ya zamani. Mahusiano ya ndoa yanataka kuachana na mahusiano ya mzazi na mtoto wake. Kwa jinsi hiyo, kuwaacha wazazi, husaidia kuambatana na mwenzi katika mahusiano ya ndoa.

2. Kuambatana.

Neno la kiebrania lililotafsiriwa kuambatana linatokana na neno lenye maana ya kushikana, kufungamana, kuungana na kushikilia. Kama nomino, hutumika pia kwa kuchomelea “kuunga” (Isa.41:7). Ukaribu unaowasilishwa na neno hili, hutumika pia katika mahusiano kati ya Mungu na watu wake. “Mche BWANA, Mungu wako, umtumikie yeye; ambatana naye, na kuapa kwa jina lake.” (Kumb.10:20).

3. Kuweka agano.

Katika maandiko, ile ahadi ambayo waliooana wanapeana huitwa agano – makubaliano makini kwenye maandiko matakatifu. (Mal.2:14; Mith.2:16, 17). Mahusiano baina ya mume na mke yapaswa kufanana na agano la Mungu la milele na watu wake ulimwenguni – kanisa. (Efe.5:21-33). Kuahidiana kwao kwapaswa kuwa kwa uaminifu ambao unaakisi uaminifu wa Mungu (Zab.89:34; Omb. 3:23). Mungu, familia za wanaofunga ndoa, na jamii inashuhudia agano ambalo ni siri. Hapa kuna umoja katika maana halisi, wafunga ndoa wanatembea pamoja, wanasimama pamoja na kushiriki uhuasiano wa ndoa. Agano hilo linaridhiwa mbinguni. “Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.” (Mt.19:6). Wanandoa wakristo huamini kwamba wamepeana agano kuwa waaminifu kwa kila moja wao hadi kifo kitakapowatenganisha.

Kuwa mwili moja.

Kuacha na kufanya agano kuambatana hufanyiza mwungano ambao ni siri. Hapa ni umoja kwa maana kamili – waliofunga ndoa hutembea pamoja, husimama pamoja na kushiriki tendo la ndoa. Mwanzoni, jambo hili huhusu mwungano wa kimwili. Kadiri maisha ya pamoja yanavyoendelea, ndipo mwungano wa mawazo na hisia hushikamana kuongezea mwungano huu wa kimwili.

a) Kutembea pamoja.

Kuhusu mahusiano yake na wanadamu, Mungu anauliza “Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana? (Amo.3:3). Swali hilo pia ni muhimu kwa wanaokuwa mwili moja. Mungu alionya Israeli wasifunge ndoa na mataifa jirani kwa sababu wangewapotosha wana wao waabudu miungu mingine. (Kumb.7:4; cf. Yosh.23:11-13). Waisraeli walipopuuza maelekezo hayo, walipatilizwa (Amu.14:16; 1Falm.11:1-10; Ezr.9:10). Paulo anarudia kanuni hii kwa mapana yake kuwa “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani gani kati ya Kristo na Beliari? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? (2Kor.6:14-18).

Ni wazi Maandiko yamekusudia waumini wafunge ndoa na wamini wenzao tu. Lakini kanuni hii inavuka ng’ambo zaidi. Umoja wa ukweli hudai kupatana juu ya imani na matendo. Tofauti ya dini hufanya mtindo wa maisha wenye migogoro na kufanya nyufa kwenye ndoa. Kuepuka hayo, Maandiko hufundisha waumini kufunga ndoa katika jamii yao wenyewe.

b) Kusimama pamoja.

Kuwa mwili moja, wawili wapaswa kuwa na utii wa imani wa kila moja kwa mwenzake. Mtu anafunga ndoa hujitahatarisha kwa yale ambayo mwenzake anakuja nayo. Wanapofunga ndoa hutangaza ukubali wao kushiriki uwajibikaji wa wenzi wao, kusimama pamoja na washiriki wao dhidi ya kila jambo. Ndoa hutaka upendo wa daima usiokata tamaa. Watu wawili hushirikiana vyote walivyo navyo, siyo tu miili yao, siyo tu mali zao; bali pia mawazo yao na hisia zao, furaha zao na huzuni zao, matumaini yao, hofu zao, mafanikio yao pamoja na kushindwa kwao. Kuwa mwili moja humaanisha wawili wanakuwa na mwili moja kikamilifu, moyo na roho moja na bado wakabaki ni nafsi mbili tofauti.

c) Tendo la ndo.

Kuwa mwili moja huhusisha mwungano wa kijinsia. “Adam akamjua Hawa mkewe naye akapata mimba.”(Mwa.4:1). Katika msukumo wao wa kuunganishwa pamoja, msukumo ambao wanaume na wanawake wana hisia nao tangu siku za Adam na Hawa, kila ndoa inayo kisa chake cha mapenzi. Kitendo cha ndoa huelezea ukaribu uliopo kuliko chochote kuhusiana na mwungano wa mwili, kihisia na kiroho. Upendo wa ndoa wa kikristo wapaswa kuwa wenye joto, furaha na kufurahiana. (Mith.5:18, 19).

Ndoa na iheshimiwe na watu wote na malazi yawe safi” (Ebr.13:4). Maandiko huelezea kuwa kitendo cha ndoa baina ya mume na mke ni mpango wa Mungu. Ni kama mwandishi wa Waebrania asemavyo siyo najisi, siyo dhambi, siyo kitendo kichafu. Ni sehemu ya heshima kubwa kwenye ndoa – patakatifu pa patakatifu ambako mume na mke hukutana peke yao kushangilia upendo kila moja kwa mwenzake. Ni wakati ambao unapaswa kuwa mtakatifu na wenye msisimko unaofurahisha.

5. Upendo ki Biblia.

Upendo wa ndoa ni upendo usio na masharti, wenye hisia na kujitoa kimwili kila mwanandoa kwa mwenzake ambao hutengeneza mazingira ya kukua pamoja katika sura na mfano wa Mungu kwa hali zote, kimwili, kihisia, kiakili na kiroho. Aina tofauti za upendo hutenda kazi katika ndoa: kuna nyakati za hisia, kuhurumia na kufariji. Pia kuna nyakati za kumilikiana katika hali zote. Hata hivyo aina ya upendo unaodumu ni ule wa agape, yaani usio wa ubinafsi, usiojitumikia ambao hujenga msingi wa upendo wa ndoa unaodumu.

Yesu alidhihirisha upendo wa hali ya juu pale alipokubali kubeba hatia na matokeo ya dhambi zetu akaenda msalabani. “Naye amewapenda watu wake katika ulimwengu, naam aliwapenda upeo” (Yoh.13:1). Alitupenda sisi pamoja na matokeo ya dhambi zetu kwake. Huu ni upendo usio na masharti wa Yesu Kristo.

Akisimulia upendo huu, Paulo anasema “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; haufurahii udhalimu; bali hufurahi pamoja na kweli; huvumilia yote; hutumaini yote; hustahimili yote. Upendo haupungui neno wakati wowote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika. (1Kor.13:4-8).

Upendo wa agape umesimikwa kwenye chanzo cha milele na hutenda kazi mahali ambako aina zingine za upendo zitashindwa. Hupenda hata kama kuna ugumu kiasi gani. Pasipo kujali kwamba mwenzi hapendeki kiasi gani wenyewe bado huchanua tu. Ni mtazamo wa kiakili unaosimamia uamuzi wa nia.

6. Uwajibikaji binafsi kwa mambo ya kiroho.

Pamoja na wanandoa kujifunga kila moja kwa mwenzake kwa njia ya agano, kila mmoja anawajibika binafsi kwa maamuzi ayafanyayo. (2Kor.5:10). Kwa maana hiyo, mwenzi hatamlaumu mwenzake kwa makosa ambayo kayafanya binafsi. Pia wapaswa kuwajibikia ukuaji binafsi wa mambo ya kiroho; hakuna atakayetegemea ustawi wa kiroho wa mwenzake kupata nguvu za kiroho. Hata hivyo, ushirikiano wa mtu na Mungu utamsaidia mwingine kuwa chanzo cha kuimarika na kumtia moyo.

Matokeo ya Kuanguka kwenye Ndoa

Kuharibika kwa sura ya Mungu kulikoletwa na dhambi kumeathiri ndoa, kama ilivyotokea kwenye maeneo mengine ya uzoefu wa mwanadamu. Ubinafsi umeingilia mahali pa upendo mkamilifu ulikotawala. Ubinafsi ni kisababishi cha msingi cha wote wasiovutwa na upendo wa Kristo. Hupinga kujitoa, utumishi na kutoa kama injili inavyotaka, na huonekana kwenye kila anguko la kikristo.

Kwa kutokutii kwao, Adam na Hawa walivunja makusudi ya kuumbwa kwao. Kabla ya dhambi waliishi kwa uwazi mbele za Mungu. Baada ya dhambi, badala ya kumjia Mungu kwa furaha, walijificha kwa hofu na kujaribu kufunika ukweli unaowahusu na kukana kuwajibika kwao kwa matendo waliyofanya. Wakiwa wamegubikwa na hatia ya dhambi, hawakuweza kukutana na jicho la Mungu na la malaika watakatifu. Ukwepaji huu wa kuwajibika na kujihesabia haki kumekuwa tabia ya mwanadamu mdhambi mbele za Mungu. Hofu iliyowafanya kufunika walilotenda, haikuharibu tu uhusiano wa Adamu na Mungu bali pia mahusiano ya wanandoa. Mungu alipowahoji, kila moja alijaribu kujitetea kwa hasara ya mwingine. Hoja zao zilionyesha kuwa upendano uliowekwa na Mungu wakati wa uumbaji ulikuwa umetoweka.

Baada ya dhambi, Mungu alimwambia mwanamke, “tamaa yako itakuwa kwa mume wako naye atakutawala. (Mwa.3:16). Alikusudia kanuni hii pasipo kuondosha ule usawa waliokuwa nao, kuwafaidia wanandoa hawa na wale watakaofuata baadaye. Ni jambo la bahati mbaya kwamba kanuni hii imepotoshwa. Toka wakati huo, utawala wa nguvu, hiana, na kuharibu utu vimewalemea wanadamu kwa uzito. Kujiangalia nafsi kumesababisha kukubaliana na kuthaminiana kupungua. Kinachofanyiza ukristo ni kurejeza sifa za ndoa ya awali. Hisia za mume na mke zapaswa kuchangia furaha ya mwenzi. Hufanyiza umoja ambao haupotezi nafsi ya mtu ambayo ni mali ya Mungu.

Kupotoka kwenye Kanuni ya Mungu

Ndoa za mwenzi zaidi ya moja.

Utaribu wa moja kuwa na wenzi wengi ni kinyume cha umoja na upamoja ambao Mungu aliuanzisha kwenye ndoa ya kwanza. Katika ndoa yenye wenzi wengi, hakuna kuacha wenzi wengine. Kwamba Maandiko husema ndoa za Wazee wa imani zilikuwa na tabia ya wenzi wengi, maelezo yake kwa uwazi husema hazikufikia kiwango cha Mungu. Vikundi viliinuka vikihujumiana katika ndoa moja (Angalia Mwa.16; cf. 29:16, 30:24 nk.) wakitumia watoto kama zana ya kihisia kuumiza washiriki wengine wa familia. Ndoa ya mwenzi moja hujenga kumilikiana na kuaminiana kunakoimarisha kupeana haki za ndoa. Wanatambua kwamba hakuna anayeweza kushiriki kile ambacho wao wanakifurahia. Ndoa ya mwenzi moja inaakisi zaidi uhusiano wa Kristo na Kanisa na baina ya mwanadamu na Mungu.

Uasherati na uzinzi.

Mawazo ya kisasa na mazoea kwa mwanandoa huhafifisha ahadi ya uaminifu kuhusu tendo la ndoa kwa mwenzake hadi kifo. Maandiko Matakatifu huhesabu tendo la ndoa nje ya ndoa kuwa ni dhambi. Usizini (Kut.20:14). Baada ya amri hii, hakuna maelezo yanayotolewa kupinga au kutetea mazoea mabaya. Maelezo kamili ya mtazamo wa kibiblia juu ya uasherati na uzinzi hupinga uvumilivu wa kisasa wa mwenendo usiofaa kwa wanandoa wanaoridhia mambo hayo. Maelezo mengi hupinga matendo hayo. (Law.20:10-12; Mith.6:24-32; 7:6-27; 1Kor.6:9, 13, 18; Gal.5:19; Efe.5:3; 1Thes.4:3; nk.).

Uasherati na uzinzi una athari mbaya kwa mtendaji na mwanandoa aliyepunjwa haki yake, kihisia, kimwili na kifedha. Huweza kuleta magonjwa ya kuambukiza na kuzaliwa watoto nje ya ndoa. Mawingu mazito ya uwongo na kukosa uaminifu hukosesha imani ya mwanandoa mtulivu kwa mwenzake. Na huenda kukosa huko imani yawezekana isirudi. Hata kama Biblia isingekemea, matokeo mabaya ya matendo maovu yangeonya juu ya tabia hii isiyofaa.

Mawazo yasiyo safi

. Dhambi siyo kile kitendo cha nje; badala yake ni jambo linaloanzia moyoni. Yesu aliona moyo kuwa na tatizo. “Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uwongo, na matukano” (Mt.15:19). Kwa kufuatisha mtazamo huu, Yesu aliona chanzo cha kukosa uaminifu kuwa ni mawazo na hisia: “Mmesikia imenenwa, Usizini; lakini mimi nawaambia, Kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.” (Mt.5: 27-28). Wanadamu wamefungua biashara kubwa kuhusu mambo ya ngono kwa mandanguro, vitabu, Internet na video ambayo haina nafasi kwenye maisha ya kikristo. Wakristo wameitwa kuwa na mawazo safi na kuishi maisha matakatifu kwa sababu wataishi maisha matakatifu kwa umilele.

Uzinzi wa mzazi kwa mtoto wake.

Baadhi ya wazazi huvuka mipaka inayotofautisha kuonyeshana hisia za upendo kwa watoto wao kwa kuwa karibu nao kwa namna isiyostahili. Mara nyingi hili hutokea wakati uhusiano wa mume na mke unapokuwa umepuuziwa. Uchafu wa aina hii ulipigwa marufuku kwenye Agano la Kale. (Law.18:6-29; Kumb.27:20-23) na kulaaniwa kwenye Agano Jipya (1Kor.5:1-5). Jambo hili huathiri maendeleo ya mtoto na itampatia aibu siku atakayoingia kwenye ndoa. Wazazi wanapokosa kwa jambo hili humvunjia mtoto imani iliyo muhimu kwa mahusiano yake na Mungu.

Talaka.

Kauli ya Yesu hujumuisha mafundisho ya Biblia kuhusu talaka. “Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.” (Mt.19:6; Mk. 10:7-9). Ndoa ni takatifu kwa sababu Mungu ameifanya iwe hivyo. Mungu amekusudia ndoa iliyofungwa isivunjike. Alipoulizwa kuhusu amri ya Musa, Yesu alijibu kuwa ni kwa sababu ya ugumu wa mioyo ila tangu mwanzo haikuwa hivyo. (Mt.19:8).

Aliendelea kusema kuwa sababu inayokubalika ya talaka ni pale mtu anapokosa uaminifu katika tendo la ndoa. (Mt.5:32; 19:9). Jibu la Yesu kwa mafarisayo linathibitisha kwamba Mungu anakusudia waliofunga ndoa kuakisi sura ya Mungu katika mwungano wa kudumu. Kukosa uaminifu kwa mwanandoa mmoja hakumaanishi lazima talaka itolewe.

Msalaba unatia moyo mtu kutubu na kusamehewa na kuondosha mizizi ya chuki. Hata kwa uzinzi, kupitia msamaha na uwezo wa Mungu wa upatanisho, mwanandoa aliyekosewa aweza kutafuta na kudumisha mpango wa asili wa Mungu. Kwa kanuni ya Biblia, uzinzi ni dhambi inayoharibu ndoa kuliko dhambi nyingine. Tunapokuwa tayari kusamehe na kuachilia hisia hasi, Mungu atakuwa tayari kuponya na kurejeza upendo kwa kila mwanandoa.

Mpango wa kimbingu kuhusu ndoa ni wa kudumu hadi kifo kitenganishe, hata hivyo wakati mwingine sheria za nchi hutoa fursa ya kutengana kutokana na ukatili kwa mwanandoa mmoja au kwa mtoto. Kutengana huko kwaweza kukawa kwa njia ya talaka tu. Kutengana huko kama haihusishi kukosa uaminifu katika tendo la ndoa, hakumpi ruhusa ya kibiblia aliyetengana kufunga ndoa nyingine. Kwa sababu ndoa ni taasisi ya kimbingu, kanisa lina jukumu kuilinda na kupinga talaka na kusaidia majeraha yake yapone kadiri inavyowezekana.

Mahusiano ya jinsia moja

Mungu aliumba mwanaume na mwanamke kutofautiana lakini kuvutiwa na kuhitaji mtu wa jinsia tofauti kwa ajili ya mahusiano yanayojenga jamii. Katika hatua nyingine, dhambi imeathiri hata jambo hili la msingi. Matokeo yake kuna mapinduzi ambayo watu wa jinsia moja huhusiana. Maandiko Matakatifu kwa nguvu nyingi hulaumu mahusiano ya jinsia moja. (Mwa.19:4-10; cf. Yud.7, 8; Law.18:22; 20:13; Rum.1:26-28; 1Tim.1:8-10). Matendo ya namna hii hupotosha sana sura ya Mungu kwa wanaume na wanawake.

Kwa sababu wote wamekosa na kupungukiwa na utukufu wa Mungu (Rum.3:23), Wakristo watashughulika ili kuwakomboa wenye mazoea ya namna hii. Watakuwa na mtazamo aliokuwa nao Yesu kwa mwanamke aliyeshikwa akizini: “Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.” (Yoh.8:11). Siyo tu kwa wenye mwelekeo wa mahusiano na wenzao wenye jinsia moja, bali wote walionaswa kwenye mazoea au mahusiano yanayosababisha mfadhaiko, aibu na kujisikia hatia huhitaji kuangaliwa na mshauri wa kikristo. Hakuna tabia iliyo ng’ambo ya uwezo wa neema ya Mungu iponyayo.

Familia

Baada ya Mungu kuwaumba Adamu na Hawa, aliwapa mamlaka ya kutawala dunia. (Mwa.1:26; 2:15). Walikuwa ni familia ya kwanza, kanisa la kwanza na ilikuwa alama ya mwanzo jamii. Kwa hiyo jamii iliundwa kwa ndoa na familia. Kwa sababu wao walikuwa ndio wanadamu wakazi pekee katika dunia, Mungu aliagiza wakazae waijaze nchi. (Mwa.1:28).

Takwimu zilizoko zadokeza kuwa sehemu ya dunia ambayo haina wakazi wanadamu haihitaji kujazwa au kutawaliwa. Lakini wanandoa wa kikristo ambao wanataka kuzaa watoto ulimwenguni wana wajibu wa kuwalea watoto wao katika njia ya BWANA, (Efe.6:4). Kabla ya wanandoa kufikiria kuzaa, wanatazamiwa kufikiri mpango wa Mungu kwa familia.

Wazazi

1. Baba.

Maandiko Matakatifu yanampa mume na baba jukumu la kuwa kiongozi na kuhani wa familia. (Kol.3:18-21; 1Pet.3:1-8). Anakuwa mfano wa Kristo, kichwa cha Kanisa. “Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.

Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji na kwa neno, apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lolote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe, hujipenda mwenyewe.” (Efe.5:23-28).

Kama Kristo anavyoliongoza kanisa, mume na mke watajitoa kila moja kwa maoni ya mwenzake lakini neno la Mungu linampa upendeleo mume kwa mambo yasiyohusu dhamiri. Wakati huo huo anapaswa kuyatendea maoni binafsi ya mkewe kwa heshima. Kama Kristo alivyojitoa kwa Kanisa, vivyo hivyo mume naye anapaswa kuongoza kwa kujitoa. Kristo hulitawala Kanisa lake kwa hekima na upendo na waume nao wapaswa kutumia madaraka yao kwa upole kama Kristo anavyotumia kuongoza Kanisa.

Akiwa kuhani wa familia, Baba ataikusanya familia yake asubuhi na kuikabidhi kwa Mungu na jioni atawaongoza kumsifu Mungu na kumshukuru kwa baraka alizotoa. Ibada ya familia itakuwa kifungo kinachoifungamanisha familia – wakati unaompa Mungu kipaumbele katika familia.

Baba mwenye hekima atatumia wakati wake na watoto. Watoto waweza kujifunza mambo mengi kwa baba yao, kama kumpenda na kumheshimu mama, upendo kwa Mungu, umuhimu wa maombi, upendo kwa watu wengine, njia ya kufanya kazi, heshima ya mavazi, kupenda maumbile ya asili na vitu ambavyo Mungu amevifanya. Ikiwa baba atakosekana nyumbani, mtoto atakosa na kunyimwa fursa muhimu na furaha.

2. Mama.

Kuwa mama ni jambo la karibu zaidi duniani la kuwa mshirika wa Mungu. Mfalme aliye kwenye kiti cha enzi hana jukumu kubwa kumpita mama. Mama ni malkia nyumbani akifanyiza tabia za watoto wake kwa umilele. Anapaswa kuitazama familia kuwa ni kazi ya maisha. Jukumu la kulea watoto siyo jukumu la kumwachia mtu ambaye hana uchungu nao.

Mungu aliweka uwezo ndani ya mama, wa kumbeba mtoto ndani ya mwili wake, kumnyonyesha, kumpenda na kumhudumia hadi atakapokuwa mtu mzima. Katika nyakati za Agano la Kale, jina lilibeba kauli fupi juu ya mwenye jina. Hawa alipokea jina lake baada ya anguko dhambini. (Mwa.3:20). Kwa sababu angewazaa wanadamu wote, jina lake kiebrania chawwah lilitokna na neno kuishi (kwa kiebrania chay). Hii inaweka cheo cha mama kuwa kisicho cha kawaida katika historia ya mwanadamu.

Kama ambavyo kuzaa halikuwa jambo la Adamu peke yake wala la Hawa peke yake vivyo hivyo malezi ya watoto halikuwa jukumu la mmoja wao pekee. Kila mzazi anao wajibu na inawapasa kulea watoto katika Bwana.

Watoto

1. Kipaumbele.

Pamoja na majukumu mengine kwa Bwana, hakuna jukumu kubwa zaidi kwa wazazi linalopita la kulea watoto waliowaleta duniani. Ustawi wa watoto lapaswa kuwa jambo la kwanza badala ya kupigania maslahi binafsi. Kwa kuwa mtoto huanza kuathirika kiakili, kiroho na kimwili kabla hajazaliwa, ustawi wao wapaswa kuangaliwa kabla mama hajajifungua.

2. Upendo.

Upendo wa mzazi kwa mtoto wapaswa kuwa usio na masharti na wenye kujinyima. Hata kama hautaakisiwa, watoto lazima waupate ili waweze kujithamini, afya ya hisia katika maisha yao yote. Watoto ambao hulazimika kuuhenyea upendo wa wazazi wao hulazimika kufanya matendo mabaya yanayoweza yakawa mazoea yenye kujenga tabia. Watoto salama kwenye upendo wa wazazi wao huweza kuwafikia wengine. Waweza kufundishwa kutoa na kupokea na sababu ya kuishi kando ya kutumikia nafsi. Kadiri wanavyokua, watajifunza kumtukuza Mungu.

3. Ahadi.

Wazazi wakristo wanawajibika kuwaweka wakfu watoto wao mapema kwa kazi ya Mungu. Kanisa la Waadventista Wasabato wanayo huduma ya namna hii ambako watoto huwekwa wakfu kama Yusufu na Mariamu walivyofanya kwa mtoto Yesu. (Luk.2:22-39). Katika huduma hii, wazazi hutoa ahadi yao kumwelimisha mtoto katika njia ya Bwana ili sura ya Mungu ifanyizwe kwa mtoto. Ili kufikia lengo hili, wazazi huwajibika kuwawahisha watoto wao kwenye Shule ya Sabato na kanisani daima na kuwafanya watoto wao kuwa sehemu ya mwili wa Kristo katika umri wao mdogo.

4. Kudumu kufundisha.

Mafundisho ya kiroho ambayo wazazi hufanya kwa watoto ni mchakato unaoendelea katika kila hatua ya maisha ya mtoto. “nawe uwafundishe watoto wakokwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo. Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako. Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako (Kumb.6:7-9; 11:18). Mivuto ya kiroho ya mtoto hufanyizwa kwa kila mazingira ya nyumbani wala siyo ibada peke yake. Itawafikia katika kumtumainia Yesu, katika mitindo yao ya maisha, mavazi, na mapambo ya nyumbani. Kumjua Mungu kama mzazi apendaye ni muhimu kwa maisha ya kikristo ya mtoto.

5. Kujifunza utiii.

“Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa Mzee.” Nidhamu ina maana pana kupita adhabu. Adhabu mara nyingi hushughulikia yaliyopita wakati nidhamu hutazama yajayo mbele. Kwenye nidhamu, mchakato humfanya mtoto awe mfuasi wa mzazi kwa ajili ya kujifunza, uongozi, na mfano wa kuiga. Humaanisha kufundisha kanuni muhimu kama utii, ukweli, haki, msimamo, uvumilivu, utaratibu, rehema, ukarimu na kutenda kazi.

Mtoto akijifunza kuwatii wazazi wake tangu udogoni, mamlaka haitakuwa jambo lenye kumsumbua kwenye maisha yake. Aina ya utii ajifunzayo mtoto ni muhimu kwa kuwa utii wa kweli huwa unafanywa siyo kwa sababu tu unatakiwa bali pia kwa sababu ni jambo linatoka moyoni. Siri ya utii wa aina hii inabeba kuzaliwa upya.

Mwanadamu anayejaribu kutii amri za Mungu kwa sababu ni wajibu, kwa sababu tu anatakiwa kufanya hivyo hataingia kwenye raha ya kutii. Utii wa kweli kunatokana na kanuni itendayo kazi kutoka moyoni. Inatokana na kupenda haki, upendo wa sheria ya Mungu. Kinachofanyiza haki ni utii kwa Mkombozi wetu. Hili hutuongoza kutenda haki kwa sababu ni vema, kwa sababu haki humpendeza Mungu.

6. Kuingia kwenye jamii na kujifunza Lugha.

Katika familia, watoto huingia kwenye jamii kama washirika wa wanadamu pamoja na majukumu yote na fursa zinazohusika. Kushirikiana ni mchakato ambao mtoto huingia ili atumikie jamii. Lugha pamoja na yahusuyo kuwasiliana ni ujuzi wa kwanza ambao mtoto hujifunza. Lugha itumikayo nyumbani yahitaji uangalizi makini, ili hatimaye imtukuze Mungu. Mtoto apaswa kusikia mara kwa mara maelezo ya furaha kwa wanafamilia na sifa kwa Mungu.

7. Kutambua jinsia.

Nyumbani, kutokana na kutenda kazi kwa wanaume na wanawake wafanyao mfumo wote wa familia, watoto hujifunza kutenda kama wanaume na wanawake ndani ya jamii. Wazazi wapaswa kuwafundisha maendeleo yao ya kijinsia kwa kuwapatia habari sahihi. Ni jukumu la wazazi pia kuwalinda watoto na matumizi mabaya ya viungo vya uzazi.

8. Kujifunza mema.

Jambo la msingi analojifunza mtoto katika kufanya ushirika na jamii ni kuzijua na kuzifuata kanuni za wema zinayothaminiwa na familia. Kile familia kinachothamini na dini huwa vinaweza kutofautiana. Wazazi wanaweza kudai kuthamini mambo kadhaa ya maisha lakini kanuni wanazoishi kwazo zikawa hazifuatishi kile wanachosema. Ni muhimu wazazi kuzingatia kutokutoa ujumbe unaogongana kwa watoto.

Familia Pana (kubwa).

Ndoa kama Mungu alivyoikusudia hutenga watu wengine, lakini familia hapana. Katika ulimwengu tulio nao ni vigumu kupata familia pana, kwamba yupo babu na bibi, ndugu wa baba wengine, wajomba na binamu kwa ukaribu. Kanisa laweza kuwapatia wale ambao mbali kupata ufahamu wa kujithamini na watu wanaoweza kuwategemea. Hapa pia mzazi moja atapata mahali pa kulea mtoto wake. Kanisa laweza kutoa vielelezo visivyopatikana nyumbani.

Kupitia kuwapenda wenye umri mkubwa walioko kwenye mkutaniko wa kanisa, watoto watajifunza kuheshimu. Wazee nao wataridhika kupata watoto wa kuwapenda na kuwafurahia. “Na hata nikiwa mzee mwenye mvi, Ee Mungu usiniache. Hata niwaeleze watu wa kizazi hiki nguvu zako. Na kila atakayekuja uweza wako.” (Zab.71:18).

Mungu hufikiria wazee kwa namna ya pekee, akisema, “Kichwa chenye mvi ni taji ya utukufu, kama kikionekana katika njia ya haki.” (Mith.16:31). Pia, “na hata uzee wenu mimi ndiye, na hata wakati wenu wa mvi nitawachukueni; nimefanya, nami nitachukua; naam, nitachukua na kuokoa.” (Isa.46:4).

Katika Kanisa, waseja watapata fursa ya kupendwa na kufurahiwa na kushiriki nguvu zao pia. Kupitia huduma yake, watatambua upendo wa Mungu kwao: “Naam, nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.” (Yer.31:3).

Ni sehemu ya “dini safi” kuangalia kwa namna ya pekee wanaohitaji msaada. (Yak.1:27; Kut. 22:22; Kumb.24:17; 26:12; Mith.23:10; Isa.1:17). Familia ya Kanisa inayo fursa kutoa kituo cha pumziko, hifadhi, mahali pa kuthaminiwa kwa wale wasio na familia; itamzingira kila mshiriki kwa umoja wa kipekee ambao Kristo alisema ndio utakaotambulisha ukristo wenyewe. (Yoh.17:20-23).

Kugeuka

Kwa kuwa familia ndiyo roho ya kanisa na jamii, familia ya Kikristo itakuwa chombo cha kuvuna roho na kutunza washiriki wake kwa Bwana. Mafungu ya mwisho ya Agano la Kale yatatimia kabla Bwana hajarejea. “Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla siku ile ya BWANA iliyo kuu na kuogofya. Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana.” (Mal.4:5, 6). Katika siku za leo, nguvu nyingi inasukuma washiriki wa familia kusambaratika waache familia. Wito wa Mungu ni wa kuunganisha tena, kuimarisha, kugeuka na kurejeza familia. Na familia zitakazosikia wito zitakuwa na nguvu ya kuushuhudia Ukristo. Makanisa yaliyofanywa kwa familia hizo yatakua, vijana wake hawataondoka na watadhihirishia ulimwengu picha njema ya Mungu.

×0001020304050607080910111213141516171819202122232425262728
Mwanzo 2:18-25X
18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye. 19 Bwana Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake. 20 Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye. 21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, 22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. 23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume. 24 Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja. 25 Nao walikuwa uchi wote wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya.
Yohana 2:1-22X
1 Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo. 2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake. 3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai. 4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia. 5 Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni. 6 Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu. 7 Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu. 8 Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka. 9 Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi, 10 akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa. 11 Mwanzo huo wa ishara Yesu aliufanya huko Kana ya Galilaya, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini. 12 Baada ya hayo akashuka mpaka Kapernaumu, yeye na mama yake na ndugu zake na wanafunzi wake; wakakaa huko siku si nyingi. 13 Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; naye Yesu akakwea mpaka Yerusalemu. 14 Akaona pale hekaluni watu waliokuwa wakiuza ng'ombe na kondoo na njiwa, na wenye kuvunja fedha wameketi. 15 Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng'ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao; 16 akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, Yaondoeni haya; msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara. 17 Wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa imeandikwa, Wivu wa nyumba yako utanila. 18 Basi Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara gani utuonyeshayo, kwamba unafanya haya? 19 Yesu akajibu, akawaambia, Livunjeni hekalu hili, nami katika siku tatu nitalisimamisha. 20 Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu? 21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake. 22 Basi alipofufuka katika wafu, wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa alisema hivi, wakaliamini lile andiko na lile neno alilolinena Yesu.
2 Wakorintho 6:14X
14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?
Waefeso 5:21-33X
21 hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo. 22 Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. 23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. 24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. 25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; 27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. 28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. 29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. 30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. 31 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. 32 Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. 33 Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.
Mathayo 5:31, 32X
31 Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka; 32 lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.
Marko 10:11, 12X
11 Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake; 12 na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini.
Luka 16:18X
18 Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini.
1 Wakorntho 7:10, 11X
10 Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe; 11 lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.
Kutoka 20:12X
12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.
Waefeso 6:1-4X
1 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki. 2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi, 3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia. 4 Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.
K. Torati 6: 5-9X
5 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote. 6 Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; 7 nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo. 8 Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako. 9 Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako.
Mithali 22:6X
6 Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.
Malaki 4: 5, 6X
5 Jipatie hekima, jipatie ufahamu; usiusahau; Wala usiyakatae maneno ya kinywa changu. 6 Usimwache, naye atakuhifadhi; Umpende, naye atakulinda.
Maathayo 19:8X
8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.
Mwanzo 1:31X
31 Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.
Mwanzo 1:26, 27X
26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.
Yohana 10:30X
30 Mimi na Baba tu umoja.
1 Wakorintho 11:3X
3 Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.
Mwanzo 1:31X
31 Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.
Mwanzo 2:20X
20 Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye.
Mwanzo 2:18X
18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
Mwanzo 2:21, 22X
21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, 22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.
Mwanzo 2:23X
23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.
1 Wakorintho 11:8X
8 Maana mwanamume hakutoka katika mwanamke, bali mwanamke katika mwanamume.
Mwanzo 2:24X
24 Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
Isaya 41:7X
7 Seremala akamtia moyo mfua dhahabu, na yeye alainishaye kwa nyundo akamhimiza yule apigaye fuawe, akiisifu kazi ya kuunga, akisema, Ni kazi njema; naye akaikaza kwa misumari isitikisike.
K. Torati 10:20X
20 Mche Bwana, Mungu wako, umtumikie yeye; ambatana naye, na kuapa kwa jina lake.
Malaki 2:14X
14 Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako.
Mithali 2:16, 17X
16 Ili kuokoka na malaya, Naam, malaya mwenye kubembeleza kwa maneno yake; 17 Amwachaye rafiki wa ujana wake, Na kulisahau agano la Mungu wake.
Waefeso 5:21-33X
21 hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo. 22 Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. 23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. 24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. 25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; 27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. 28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. 29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. 30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. 31 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. 32 Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. 33 Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.
Zaburi 89:34X
34 Mimi sitalihalifu agano langu, Sitalibadili neno lililotoka midomoni mwangu.
Maombolezo 3:23X
23 Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu.
Mathayo 19:6X
6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
Amos 3:3X
3 Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?
K. Torati 7:4X
4 Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya Bwana juu yenu, naye atakuangamiza upesi.
Yoshua 23:11-13X
11 Jihadharini nafsi zenu, basi, ili mmpende Bwana, Mungu wenu. 12 Lakini mkirudi nyuma kwa njia yo yote na kushikamana na mabaki ya mataifa, yaani, mataifa haya yaliyobaki kati yenu, na kuoana nao, na kuingia kwao, nao kuingia kwenu; 13 jueni hakika ya kuwa Bwana, Mungu wenu, hatawafukuza tena mataifa haya mbele ya macho yenu, bali watakuwa mtego kwenu na tanzi, na mjeledi mbavuni mwenu, na miiba machoni mwenu, hata mtakapoangamia na kutoka katika nchi hii njema, ambayo Bwana, Mungu wenu, amewapa ninyi.
Waamuzi 14:16X
16 Basi mkewe Samsoni akalia mbele yake, akasema, Wewe wanichukia tu, wala hunipendi; wewe umewategea kitendawili hao wana wa watu wangu, nawe hukuniambia mimi. Naye akamwambia, Angalia, sikumwambia baba yangu wala mama yangu, nami nikuambie wewe?
1 Wafalme 11:1-10X
1 Mfalme Sulemani akawapenda wanawake wengi wageni, pamoja na binti yake Farao, wanawake wa Wamoabi, na wa Waamoni, na wa Waedomi, na wa Wasidoni, na wa Wahiti, 2 na wa mataifa Bwana aliyowaambia wana wa Israeli, Msiingie kwao, wala wasiingie kwenu; kwa kuwa hakika wataigeuza mioyo yenu kuifuata miungu yao. Sulemani akaambatana nao kwa kuwapenda. 3 Akawa na wake mia saba binti za kifalme, na masuria mia tatu; nao wakeze wakamgeuza moyo. 4 Maana ikawa, Sulemani alipokuwa mzee, wake zake wakamgeuza moyo wake, afuate miungu mingine, wala moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana, Mungu wake, kama moyo wa Daudi baba yake. 5 Kwa kuwa Sulemani akamfuata Ashtorethi, mungu mke wa Wasidoni na Milkomu, chukizo la Waamoni. 6 Sulemani akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wala hakumfuata Bwana kwa utimilifu, kama Daudi baba yake. 7 Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni. 8 Na kadhalika ndivyo alivyowafanyia wake zake wa nchi za kigeni, waliofukiza uvumba, wakawatolea miungu yao dhabihu. 9 Basi Bwana akamghadhibikia Sulemani kwa sababu moyo wake umegeuka, naye amemwacha Bwana, Mungu wa Israeli, aliyemtokea mara mbili, 10 akamwamuru katika habari ya jambo lilo hilo asifuate miungu mingine; lakini yeye hakuyashika aliyoyaamuru Bwana.
Ezra 9:10X
10 Na sasa, Ee Mungu wetu, tuseme nini baada ya hayo? Maana tumeziacha amri zako,
2 Wakorintho 6:14-18X
14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? 15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini? 16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. 18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,
Mwanzo 4:1X
1 Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa Bwana.
Mithali 5:18, 19X
18 Chemchemi yako ibarikiwe; Nawe umfurahie mke wa ujana wako. 19 Ni ayala apendaye na paa apendezaye; Maziwa yake yakutoshe sikuzote; Na kwa upendo wake ushangilie daima.
Waebrania 13:4X
4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.
Yohana 13:1X
1 Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo.
1 Wakorintho 13:4-8X
4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; 6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; 7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. 8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
2 Wakorintho 5:10X
10 Kwa maana imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya.
Mwanzo 3:16X
16 Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.
Mwanzo 16X
1 Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, jina lake Hajiri. 2 Sarai akamwambia Abramu, Basi sasa, Bwana amenifunga tumbo nisizae, umwingilie mjakazi wangu labda nitapata uzao kwa yeye. Abramu akaisikiliza sauti ya Sarai. 3 Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe. 4 Basi akamwingilia Hajiri, naye akapata mimba. Naye alipoona ya kwamba amepata mimba, bibi yake alikuwa duni machoni pake. 5 Sarai akamwambia Abramu, Ubaya ulionipata na uwe juu yako; nimekupa mjakazi wangu kifuani mwako, naye alipoona kwamba amepata mimba, mimi nimekuwa duni machoni pake. Bwana na ahukumu kati ya mimi na wewe. 6 Naye Abramu akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mkononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake. 7 Malaika wa Bwana akamwona kwenye chemchemi ya maji katika jangwa, chemchemi iliyoko katika njia ya kuendea Shuri. 8 Akamwambia, Hajiri, wewe mjakazi wa Sarai, unatoka wapi, nawe unakwenda wapi? Akanena, Nakimbia mimi kutoka mbele ya bibi yangu Sarai. 9 Malaika wa Bwana akamwambia, Rudi kwa bibi yako, ukanyenyekee chini ya mikono yake. 10 Malaika wa Bwana akamwambia, Hakika nitauzidisha uzao wako, wala hautahesabika kwa jinsi utakavyokuwa mwingi. 11 Malaika wa Bwana akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana Bwana amesikia kilio cha mateso yako. 12 Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote. 13 Akaliita jina la Bwana aliyesema naye, Wewe U Mungu uonaye, kwani alisema, Hata hapa nimemwona yeye anionaye? 14 Kwa hiyo kisima kile kiliitwa Beer-lahai-roi.Tazama,kiko kati ya kadeshi na beredi. 15 Hajiri akamzalia Abramu mwana wa kiume; Abramu akamwita jina lake Ishmaeli, yule mwanawe, ambaye Hajiri alimzaa. 16 Naye Abramu alikuwa mtu wa miaka themanini na sita, hapo Hajiri alipomzalia Abramu Ishmaeli.
Mwanzo 29:16X
16 Labani alikuwa na binti wawili, jina la mkubwa ni Lea, na jina la mdogo ni Raheli.
Mwanzo 30:24X
24 Akamwita jina lake Yusufu, akisema, Bwana aniongeze mwana mwingine.
Kutoka 20:14X
14 Usizini.
M. Walawi 20:10-12X
10 Na mtu aziniye na mke wa mtu mwingine, naam, yeye aziniye na mke wa jirani yake, mtu mume aziniye, na mwanamke aziniye, hakika watauawa.
Mithali 6:24-32X
24 Yakulinde na mwanamke mwovu, asikupate, Na kukuponya na ubembelezi wa mgeni. 25 Usiutamani uzuri wake moyoni mwako; Wala usikubali akunase kwa kope za macho yake. 26 Maana kwa malaya mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate; Na kahaba humwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani 27 Je! Mtu aweza kuua moto kifuani pake, Na nguo zake zisiteketezwe? 28 Je! Mtu aweza kukanyaga makaa ya moto, Na nyayo zake zisiungue? 29 Ndivyo alivyo aingiaye kwa mke wa jirani yake; Kila mtu amgusaye huyo atakuwa na hatia. 30 Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha, iwapo aona njaa; 31 Lakini akipatikana, atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake. 32 Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.
Mithali 7:6-27X
6 Maana katika dirisha la nyumba yangu Nalichungulia katika shubaka yake; 7 Nikaona katikati ya wajinga, Nikamtambua miongoni mwa vijana, Kijana mmoja asiyekuwa na akili, 8 Akipita njiani karibu na pembe yake, Akiishika njia iendayo nyumbani kwake, 9 Wakati wa magharibi, wakati wa jioni, Usiku wa manane, gizani. 10 Na tazama, mwanamke akamkuta, Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo; 11 Ana kelele, na ukaidi; Miguu yake haikai nyumbani mwake. 12 Mara yu katika njia kuu, mara viwanjani, Naye huotea kwenye pembe za kila njia. 13 Basi akamshika, akambusu, Akamwambia kwa uso usio na haya, 14 Kwangu ziko sadaka za amani; Leo hivi nimeziondoa nadhiri zangu; 15 Ndiyo maana nikatoka nikulaki, Nikutafute uso wako kwa bidii, nami nimekuona. 16 Nimetandika kitanda changu, magodoro mazuri, Kwa matandiko ya Kimisri yenye mistari. 17 Nimetia kitanda changu manukato, Manemane na udi na mdalasini. 18 Haya, na tushibe upendo hata asubuhi, Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba. 19 Maana mume wangu hayumo nyumbani, Amekwenda safari ya mbali; 20 Amechukua mfuko wa fedha mkononi; Atarudi wakati wa mwezi mpevu. 21 Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi, Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda. 22 Huyo akafuatana naye mara hiyo, Kama vile ng'ombe aendavyo machinjoni; Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu; 23 Hata mshale umchome maini; Kama ndege aendaye haraka mtegoni; Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake. 24 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Mkayaangalie maneno ya kinywa changu. 25 Moyo wako usizielekee njia zake, Wala usipotee katika mapito yake. 26 Maana amewaangusha wengi waliojeruhi, Naam, jumla ya waliouawa naye ni jeshi kubwa. 27 Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti.
1 Wakorintho 6:9, 13, 18X
9 Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, 13 Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. Lakini mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili. 18 Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.
Wagalatia 5:19X
19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
Waefeso 5:3X
3 Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;
1 Wathesalonike 4:3X
3 Lakini, kwangu mimi, si kitu kabisa nihukumiwe na ninyi, wala kwa hukumu ya kibinadamu, wala sijihukumu hata nafsi yangu.
Mathayo 15:19X
19 Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni.
Mathayo 5: 27-28X
27 Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; 28 lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.
M. Walawi 18:6-29X
6 Mtu ye yote aliye wa kwenu asimkaribie mwenziwe aliye wa jamaa yake ya karibu ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana. 7 Utupu wa baba yako, wala utupu wa mama yako, usifunue, maana ndiye mama yako; usifunue utupu wake. 8 Utupu wa mke wa baba yako, usifunue; maana, ni utupu wa baba yako. 9 Utupu wa umbu lako, binti ya baba yako, au binti ya mama yako, kwamba alizaliwa nyumbani mwenu au kwamba alizaliwa kwengine, utupu wa hao usifunue. 10 Utupu wa binti ya mwanao mume, au wa binti ya binti yako, utupu wao hao usifunue; kwa kuwa ndio utupu wako mwenyewe. 11 Utupu wa binti ya mkewe baba yako, aliyezaliwa na baba yako, yeye ni umbu lako, usifunue utupu wake. 12 Usifunue utupu wa umbu lake baba yako; maana, yeye ni jamaa aliye karibu. 13 Usifunue utupu wa umbu la mama yako; maana, yeye ni jamaa ya mama yako ya karibu. 14 Usifunue utupu wa ndugu ya baba yako, usimkaribie mkewe huyo; yeye ni shangazi lako. 15 Usifunue utupu wa mkweo mwanamke; yeye ni mke wa mwanao; usifunue utupu wake huyo. 16 Usifunue utupu wa mke wa nduguyo; maana, ni utupu wa nduguyo. 17 Usifunue utupu wa mwanamke na binti yake; usimtwae binti ya mwanawe mume, au binti ya binti yake, ili kufunua utupu wake; hao ni jamaa ya karibu; ni uovu mkuu. 18 Wala usitwae mwanamke pamoja na nduguye, awe mtesi wake, na kufunua utupu wake, huyo wa pili atakapokuwa yu hai. 19 Nawe usimkaribie mwanamke kufunua utupu wake wakati wa kutengwa kwa ajili ya unajisi wake. 20 Usilale na mke wa mwenzio, ukajitia unajisi naye. 21 Nawe usitoe kizazi chako cho chote na kuwapisha kwa Moleki, wala usilinajisi jina la Mungu wako; mimi ndimi Bwana. 22 Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo. 23 Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; ni uchafuko. 24 Msijitie unajisi katika mambo hayo hata mojawapo; kwa maana hizo taifa nitakazozitoa mbele zenu zimekuwa najisi kwa mambo hayo yote; 25 na hiyo nchi imekuwa najisi; kwa ajili ya hayo naipatiliza uovu wake juu yake, na hiyo nchi yatapika wenyeji wake na kuwatoa. 26 Kwa hiyo mtazishika amri zangu na hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala mgeni aketiye kati yenu; 27 (kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;) 28 ili kwamba hiyo nchi isiwatapike na ninyi pia, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu. 29 Kwani mtu awaye yote atakayefanya machukizo hayo mojawapo, nafsi hizo zitakazoyafanya zitakatiliwa mbali na watu wao.
K. Torati 27:20-23X
20 Na alaaniwe alalaye na mke wa baba yake, kwa kuwa amefunua mavazi ya babaye. Na watu wote waseme, Amina. 21 Na alaaniwe alalaye na mnyama wa aina yo yote. Na watu wote waseme, Amina. 22 Na alaaniwe alalaye na umbu lake, binti ya babaye, au binti ya mamaye. Na watu wote waseme, Amina. 23 Na alaaniwe alalaye na mkwewe, mamaye mkewe. Na watu wote waseme, Amina.
1 Wakorintho 5:1-5X
1 Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye. 2 Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo. 3 Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo. 4 Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu; 5 kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu.
Mathayo 19:6X
6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
Marko 10:7-9X
7 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; 8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. 9 Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.
Mathayo 19:8X
8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.
Mathayo 5:32X
32 lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.
Mathayo 19:9X
9 Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.
Mwanzo 19:4-10X
4 Hata kabla hawajalala, watu wa mji, wenyeji wa Sodoma, wakaizunguka nyumba, vijana kwa wazee, watu wote waliotoka pande zote. 5 Wakamwita Lutu, wakamwambia, Wa wapi wale watu waliokuja kwako usiku huu? Uwatoe kwetu, tupate kuwajua. 6 Lutu akawatokea mlangoni, akafunga mlango nyuma yake. 7 Akasema, Basi, nawasihi, ndugu zangu, msitende vibaya hivi. 8 Tazama, ninao binti wawili ambao hawajajua mtu mume, nawasihi nitawatolea kwenu mkawafanyie vilivyo vyema machoni penu, ila watu hawa msiwatende neno, kwa kuwa wamekuja chini ya dari yangu. 9 Wakasema Ondoka hapa! Kisha wakanena, Mtu huyu mmoja amekuja kwetu kuketi hali ya ugeni; naye kumbe, anataka kuhukumu! Basi tutakutenda wewe vibaya kuliko hawa. Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, wakakaribia wauvunje mlango. 10 Lakini wale watu wakanyosha mikono yao, wakamwingiza Lutu kwao nyumbani, wakaufunga mlango.
Yuda 1:7, 8X
7 Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele. 8 Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu.
M. Walawi 18:22X
22 Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo.
M. Walawi 20:13X
13 Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume, kama alalavyo na mtu mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.
Warumi 1:26-28X
26 Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; 27 wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao. 28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.
1 Timotheo 1:8-10X
8 Lakini twajua ya kuwa sheria ni njema, kama mtu akiitumia kwa njia iliyo halali; 9 akilifahamu neno hili, ya kuwa sheria haimhusu mtu wa haki, bali waasi, na wasio wataratibu, na makafiri, na wenye dhambi, na wanajisi, na wasiomcha Mungu, na wapigao baba zao, na wapigao mama zao, na wauaji, 10 na wazinifu, na wafiraji, na waibao watu, na waongo, nao waapao kwa uongo; na likiwapo neno lo lote linginelo lisilopatana na mafundisho yenye uzima;
Warumi 3:23X
23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
Yohana 8:11X
11 Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.
Mwanzo 1:26X
26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
Mwanzo 2:15X
15 Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.
Mwanzo 1:28X
28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.
Waefeso 6:4X
4 Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana.
Wakolosai 3:18-21X
18 Ninyi wake, watiini waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana. 19 Ninyi waume, wapendeni wake zenu msiwe na uchungu nao. 20 Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana. 21 Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.
1 Petro 3:1-8X
1 Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi; 4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu. 5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao. 6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote. 7 Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe. 8 Neno la mwisho ni hili; mwe na nia moja, wenye kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitikivu, wanyenyekevu;
Waefeso 5:23-28X
23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. 24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. 25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; 27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. 28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
Mwanzo 3:20X
20 Adamu akamwita mkewe jina lake Hawa; kwa kuwa yeye ndiye aliye mama yao wote walio hai.
Luka 2:22-39X
22 Kisha, zilipotimia siku za kutakasika kwao, kama ilivyo torati ya Musa walikwenda naye hata Yerusalemu, wamweke kwa Bwana, 23 (kama ilivyoandikwa katika sheria ya Bwana, Kila mtoto mwanamume aliye kifungua mimba ya mamaye na aitwe mtakatifu kwa Bwana), 24 wakatoe na sadaka, kama ilivyonenwa katika sheria ya Bwana, Hua wawili au makinda ya njiwa wawili. 25 Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. 26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana. 27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria, 28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema, 29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema; 30 Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako, 31 Uliouweka tayari machoni pa watu wote; 32 Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli. 33 Na babaye na mamaye walikuwa wakiyastaajabia hayo yaliyonenwa juu yake. 34 Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, Tazama, huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi walio katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa. 35 Nawe mwenyewe, upanga utaingia moyoni mwako, ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi. 36 Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake. 37 Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba. 38 Huyu alitokea saa ile ile akamshukuru Mungu, na wote waliokuwa wakiutarajia ukombozi katika Yerusalemu akawatolea habari zake. 39 Basi, walipokwisha kuyatimiza yote kama yalivyoagizwa katika sheria ya Bwana, walirejea Galilaya mpaka mjini kwao, Nazareti.
K. Torati 6:7-9X
7 nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo. 8 Yafunge yawe dalili juu ya mkono wako, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yako. 9 Tena yaandike juu ya miimo ya nyumba yako, na juu ya malango yako.
K. Torati 11:18X
18 Kwa hiyo yawekeni maneno yangu mioyoni mwenu na rohoni mwenu; yafungeni yawe dalili juu ya mikono yenu, nayo yatakuwa kama utepe katikati ya macho yenu.
Zaburi 71:18X
18 Na hata nikiwa ni mzee mwenye mvi, Ee Mungu, usiniache. Hata niwaeleze watu wa kizazi hiki nguvu zako, Na kila atakayekuja uweza wako.
Mithali 16:31X
31 Kichwa chenye mvi ni taji ya utukufu, Kama kikionekana katika njia ya haki.
Isaya 46:4X
4 na hata uzee wenu mimi ndiye, na hata wakati wenu wa mvi nitawachukueni; nimefanya, nami nitachukua; naam, nitachukua na kuokoa.
Yeremia 31:3X
3 Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.
Yakobo 1:27X
27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.
Kutoka 22:22X
22 Usimtese mjane ye yote aliyefiwa na mumewe, wala mtoto yatima.
K. Torati 24:17X
17 Usipotoshe hukumu ya mgeni, wala ya yatima; wala usitwae mavazi ya mjane, yawe rehani;
K. Torati 26:12X
12 Utakapokwisha kutoa zaka, katika zaka zote za maongeo yako mwaka wa tatu, ambao ndio mwaka wa kutolea zaka, umpe zile zaka Mlawi, na mgeni, na yatima, na mjane, wapate kula ndani ya malango yako na kushiba;
Mithali 23:10X
10 Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani; Wala usiingie katika mashamba ya yatima;
Isaya 1:17X
17 jifunzeni kutenda mema; takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane.
Yohana 17:20-23X
20 Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao. 21 Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. 22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja. 23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.
Malaki 4:5, 6X
5 Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya. 6 Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana.