Karama za Roho na Huduma

Utangulizi


Mojawapo ya karama za Roho Mtakatifu ni unabii. Karama hii ni alama inayolitambulisha masalio na ilidhihirika katika huduma ya Ellen G. White. Kama mjumbe wa Bwana, maandishi yake yanaendelea kuwa chanzo madhubuti cha ukweli yanayotoa kwa kanisa faraja, uongozi, mafundisho, na maonyo. Pia yanaweka wazi kwamba Biblia ndiyo kanuni ambayo kwayo mafundisho yote na uzoefu lazima vipimwe.” (Yoe. 2:28, 29;
Yoeli 2:28,29;X
28 Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono; 29 tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu.
Mdo. 2: 14-21
Matendo 2:14-21X
14 Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake. 15 Siku zile akasimama Petro kati ya hao ndugu (jumla ya majina ilipata mia na ishirini), akasema, 16 Ndugu, ilipasa andiko litimizwe, alilolinena Roho Mtakatifu zamani kwa kinywa cha Daudi, katika habari za Yuda aliyewaongoza wao waliomkamata Yesu; 17 kwa sababu alikuwa amehesabiwa pamoja na sisi, akapata sehemu ya huduma hii. 18 (Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka. 19 Ikajulikana na watu wote wakaao Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde la damu.) 20 Kwa maana imeandikwa katika chuo cha Zaburi, Kikao chake na kiwe ukiwa, Wala asiwepo mtu mwenye kukaa humo; 21 Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu,
Ebr. 1: 1-3;
Waebrania 1:1-3;X
1 Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, 2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. 3 Yeye kwa kuwa ni mng'ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu;
Ufu. 12:17;
Ufunuo 12:17X
17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.
Uf. 19:10)
Ufunuo 19:10X
10 Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.

Manabii walitekeleza jukumu muhimu kwenye nyakati za Agano la Kale na Agano Jipya. Je, unabii utakoma baada ya Biblia kuandikwa? Ili kupata jibu, ni vema tukapitia historia ya manabii.

Karama ya Unabii nyakati za Biblia

Ijapokuwa dhambi ilikomesha mawasiliano ya moja kwa moja baina ya Mungu na wanadamu (Isa. 59:1,2;

Isaya 59:1,2;X
1 Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; 2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.
Kut. 20:18),
Kutoka 20:18X
18 Watu wote wakaona umeme na ngurumo na sauti ya baragumu, na ule mlima kutoka moshi; na watu walipoona hayo wakatetemeka, wakasimama mbali.
Mungu hakukoma kuwasiliana na wanadamu. Alianzisha namna nyingine ya kuwasiliana na wanadamu kwa kupitia manabii (Ebr. 1:1-3,
Waebrania 1:1-3,X
1 Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, 2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. 3 Yeye kwa kuwa ni mng'ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu;
Uf. 1:1;
Ufunuo 1:1X
1 Ufunuo wa Yesu Kristo, aliopewa na Mungu awaonyeshe watumwa wake mambo ambayo kwamba hayana budi kuwako upesi; naye akatuma kwa mkono wa malaika akamwonyesha mtumwa wake Yohana;
Hes. 12:6)
Hesabu 12:6X
6 Kisha akawaambia,Sikizeni basi maneno yangu;Akiwapo nabii kati yenu,Mimi,Bwana,nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto.
. Katika Maandiko Matakatifu, nabii ni mtu ambaye hupokea mawasiliano kutoka kwa Mungu na kuwasilisha maudhui yake kwa watu wake Mungu. “Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu (2Pet. 1:21)
2 Petro 1:21X
21 Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
Katika Agano la Kale, tafsiri ya nabii inatokana na neno la kiebrania nabi pale Mungu alipomwambia Musa kuwa amemweka kama Mungu kwa Farao na Haruni atakuwa nabii (Kut. 7: 1, 2).
Kutoka 7:1,2X
1 Bwana akamwambia Musa, Angalia, nimekufanya wewe kuwa kama Mungu kwa Farao; na huyo ndugu yako Haruni atakuwa nabii wako. 2 Utanena hayo yote nikuagizayo; na ndugu yako Haruni atanena na Farao, ili awape wana wa Israeli ruhusa watoke nchi yake.
Majina mengine ni roeh (Isa. 30:10)
Isaya 30:10X
10 wawaambiao waonaji, Msione; na manabii, Msitoe unabii wa mambo ya haki, tuambieni maneno laini, hubirini maneno yadanganyayo;
au chozeh (2Sam. 24:11;
2 Samweli 24:11X
11 Na Daudi alipoondoka asubuhi, neno la Bwana likamjia nabii Gadi, mwonaji wake Daudi, kusema,
2 Falme 17:13).
2 Wafalme 17:13X
13 Pamoja na hayo Bwana aliwashuhudia Israeli, na Yuda, kwa kinywa cha kila nabii, na cha kila mwonaji, akisema, Geukeni, na kuziacha njia zenu mbaya, mkazishike amri zangu na hukumu zangu, sawasawa na ile sheria yote niliyowaamuru baba zenu, nikawapelekea kwa kinywa cha manabii watumishi wangu.
Zamani katika Israel mtu alipokwenda kuuliza jambo kwa Bwana alisema tukamwone mwonaji (1Sam.9:9)
1 Samweli 9:9X
9 (Hapo zamani katika Israeli, mtu alipokwenda kuuliza neno kwa Mungu, husema hivi, Haya! Twende kwa mwonaji; maana mtu aitwaye sasa Nabii hapo zamani aliitwa Mwonaji.)
. Neno ‘mwonaji’ hukazia kwamba mtu hupokea ujumbe kutoka kwa Mungu. Kwa miaka mingi, Mungu amekuwa akiwasiliana na mwanadamu kwa njia na manabii (Amo. 3:7).
Amosi 3:7X
7 Hakika Bwana MUNGU hatafanya neno lo lote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.

Majukumu ya Manabii katika Agano Jipya

  1. Kusaidia Kuanzisha Kanisa:Kanisa limejengwa kwa msingi wa mitume na manabii, Yesu Kristo akiwa jiwe kuu la pembeni (Efe.2:20,21).
    Waefeso 2:20,21X
    20 aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; 21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;
  2. Walianzisha Utume wa Kanisa: Ni kwa njia ya manabii, Roho Mtakatifu aliwachagua Paulo na Barnaba kwa safari yao ya kwanza ya kiutume (Mdo. 13:1, 2)
    Matendo 13:1,2X
    1 Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli. 2 Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.
    na akaelekeza ni wapi waende kufanya kazi (Mdo.16:6-10)
    Matendo 16:6-10X
    6 Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia. 7 Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa, 8 wakapita Misia wakatelemkia Troa. 9 Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie. 10 Basi alipokwisha kuyaona yale maono, mara tukataka kutoka kwenda Makedonia, kwa kuwa tuliona hakika ya kwamba Mungu ametuita tuwahubiri Habari Njema.
  3. Walijenga kanisa kiroho: Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji (1Kor.14:3)
    1 Wakorintho 14:3X
    3 Bali yeye ahutubuye, asema na watu maneno ya kuwajenga, na kuwafariji, na kuwatia moyo.
    . Pamoja na karama zingine za roho, unabii umetolewa kusudi la kuwakamilisha watakatifu kwa ajili ya kazi za huduma, ili kwamba mwili wa Kristo upate kujengwa.(Efe.4:12)
    Waefeso 4:12X
    12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe;
  4. Waliunganisha na kulilinda kanisa: Manabii walisaidia umoja wa imani na kulilinda na mafundisho ya uwongo mpaka sote tutakapoufikia umoja katika imani na katika kumjua sana Mwana wa Mungu na kuwa watu wazima kwa kufikia kipimo cha ukamilifu wa Kristo. Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwatupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa mafundisho kwa hila za watu, kwa ujanja, kwa kufuata njia zao za udanganyifu.(Efe.4:13,14)
    Waefeso 4:13,14X
    13 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo; 14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu.
  5. Walionya juu ya hatari zijazo: Nabii moja katika Agano Jipya alionya juu ya njaa itakayokumba watu karibuni (Mdo.11:27-30)
    Matendo 11:27-30X
    27 Siku zizo hizo manabii walitelemka kutoka Yerusalemu hata Antiokia. 28 Na tulipokusanyika akasimama mmoja wao, jina lake Agabo, akaonyesha kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itakuja karibu katika dunia nzima, nayo ikatukia katika siku za Klaudio. 29 Na wale wanafunzi, kila mtu kwa kadiri ya alivyofanikiwa, wakaazimu kupeleka msaada kwa ndugu zao waliokaa Uyahudi. 30 Wakafanya hivyo, wakawapelekea wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli.
    na wengine walionya kwamba Paulo atakamatwa na kufungwa Yerusalemu (Mdo. 20:23, 21:4, 10-14)
    Matendo 20:23,21:4,20-14X
    23 isipokuwa Roho Mtakatifu mji kwa mji hunishuhudia akisema, ya kwamba vifungo na dhiki vyaningoja. 4 Tukiisha kuwaona wanafunzi tukakaa huko siku saba, nao wakamwambia Paulo kwa uweza wa Roho asipande kwenda Yerusalemu. 14 Alipotufikia huko Aso, tukampakia, kisha tukafika Mitilene.
  6. Walithibitisha imani wakati wa ushindani: Baada ya baraza la kanisa kuamua juu ya hoja za wokovu wa mataifa mengine, manabi walitumwa kwenda kuimarisha waumini. “Yuda na Sila, ambao wenyewe walikuwa manabii wakanena maneno mengi ya kuwatia moyo na kuwajenga katika imani wale ndugu walioamini.” (Mdo. 15:32)
    Matendo 15:32X
    32 Tena Yuda na Sila, kwa kuwa wao wenyewe ni manabii, wakawausia ndugu kwa maneno mengi, wakawathibitisha.

Karama ya Unabii katika Siku za Mwisho

Wengi huamini kwamba karama ya unabii ilikoma wakati wa mitume kwenye Agano Jipya. Hata hivyo Biblia huthibitisha kuwepo kwa karama hii wakati wa taabu, siku za mwisho.

Kuendelea kwa karama ya unabii

Hakuna ushahidi kwamba Mungu ataondosha karama ya unabii iliyotolewa kujenga kanisa (Efe.4:13)

Waefeso 4:13X
13 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;
Paulo alionya watu wasimzimishe Roho na kupima unabii (1Thes.5:19, 20).
1 Wathesalonike 5:19,20X
19 Msimzimishe Roho; 20 msitweze unabii;
Akahimiza watu wapate kuhutubu (1Kor.14:1).
1 Wakorintho 14:1X
1 Ufuateni upendo, na kutaka sana karama za rohoni, lakini zaidi kwamba mpate kuhutubu.
Kukosekana kwa karama hii hakumaanishi kwamba Mungu amekoma kuzungumza na Kanisa bali kuwepo kwake kumeimarisha washiriki wakati wa taabu.

Karama ya Unabii karibu na Kuja kwa Yesu mara ya Pili

Kama alivyotoa karama ya unabii kwa Yohana Mbatizaji amtambulishe Yesu kwa wanadamu, Mungu atatoa karama ya unabii ili kuja kwa Yesu mara ya pili kutangazwe kwa nguvu. Ni ukweli kwamba Yesu alitabiri ujio wa manabii wa uongo kabla ya ujio wake (Mt. 24:11, 24)

Mathayo 24:11,24X
11 Na manabii wengi wa uongo watatokea, na kudanganya wengi. 12 Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa. 13 Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka. 14 Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja. 15 Basi hapo mtakapoliona chukizo la uharibifu, lile lililonenwa na nabii Danieli, limesimama katika patakatifu (asomaye na afahamu), 16 ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani; 17 naye aliye juu ya dari asishuke kuvichukua vitu vilivyomo nyumbani mwake; 18 wala aliye shambani asirudi nyuma kuichukua nguo yake. 19 Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo! 20 Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato. 21 Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe. 22 Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo. 23 Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki. 24 Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule.
na hili huashiria kwamba watakuwepo manabii wa kweli pia. Nabii Yoeli alitabiri kuwepo kwa ujazo wa Roho Mtakatifu ambao utatambulisha karama hii (Yoe. 2:28-31).
Yoeli 2:28-31X
28 Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono; 29 tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu. 30 Nami nitaonyesha mambo ya ajabu katika mbingu na katika dunia, damu, na moto, na minara ya moshi. 31 Jua litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla haijaja hiyo siku ya Bwana iliyo kuu na itishayo.
Petro aliutumia unabii huu siku ya Pentekoste (Mdo. 2:2-21).
Matendo 2:2-21X
2 Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. 3 Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. 4 Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka. 5 Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. 6 Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe. 7 Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? 8 Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo? 9 Warparthi na Wamedi na Waelami, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia, 10 Frigia na Pamfilia, Misri na pande za Libia karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na waongofu, 11 Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu. 12 Wakashangaa wote wakaingiwa na shaka, wakiambiana, Maana yake nini mambo haya? 13 Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya. 14 Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu. 15 Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana; 16 lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli, 17 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto. 18 Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri. 19 Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi. 20 Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri. 21 Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.
Mvua ya masika hukomaza mazao (Yoeli 2:23)
Yoeli 2:23X
23 Furahini, basi, enyi wana wa Sayuni, mkamfurahie Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa yeye huwapa ninyi mvua ya masika, kwa kipimo cha haki, naye huwanyeshea mvua, mvua ya masika, na mvua ya vuli, kama kwanza.
na kwa hiyo, ujio wa Roho Mtakatifu mwisho wa wakati utaimarisha imani (cf. Mt. 24:29;
Mathayo 24:29X
29 Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;
Uf. 6;12-17,
Ufunuo 6:12-17,X
12 Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu. 13 Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume. 14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo. 15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule. 16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake. 17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.
Yoe. 2:31,
Yoeli 2:31,X
31 Jua litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla haijaja hiyo siku ya Bwana iliyo kuu na itishayo.
Mt. 13:30, 39;)
Mathayo 13:30,39X
30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu. 31 Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake; 32 nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake. 33 Akawaambia mfano mwingine; Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachachwa wote pia. 34 Hayo yote Yesu aliwaambia makutano kwa mifano; wala pasipo mfano hakuwaambia neno; 35 ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema, Nitafumbua kinywa changu kwa mifano, Nitayatamka yaliyositirika tangu awali. 36 Kisha Yesu akawaaga makutano, akaingia nyumbani; wanafunzi wake wakamwendea, wakasema, Tufafanulie mfano wa magugu ya kondeni. 37 Akajibu, akasema, Azipandaye zile mbegu njema ni Mwana wa Adamu; 38 lile konde ni ulimwengu; zile mbegu njema ni wana wa ufalme; na yale magugu ni wana wa yule mwovu; 39 yule adui aliyeyapanda ni Ibilisi; mavuno ni mwisho wa dunia; na wale wavunao ni malaika.
na yeyote atakayeliitia jina la Bwana ataokoka (Yoe.2:32)

Karama ya Unabii katika Kanisa la Masalio

Ufunuo 12 kinaonyesha vipindi viwili vya mateso kwa watu wa Mungu. Kipindi cha kwanza ni kile cha miaka 1260 ya mtu wa kuasi (Uf.12:6, 14).

Ufunuo 12:6,14X
6 Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na Mungu, ili wamlishe huko muda wa siku elfu na mia mbili na sitini. 7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; 8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. 9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye. 10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. 11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa. 12 Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu. 13 Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume. 14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.
Kabla ya Yesu kurudi, masalio wenye kushika amri za Mungu na wenye ushuhuda wa Yesu watakasirikiwa na Shetani (Uf.12:17
Ufunuo 12:17 X
17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.
cf. Dan.12:1).
Danieli 12:1X
1 Wakati huo Mikaeli atasimama, jemadari mkuu, asimamaye upande wa wana wa watu wako; na kutakuwa na wakati wa taabu, mfano wake haukuwapo tangu lilipoanza kuwapo taifa hata wakati uo huo; na wakati huo watu wako wataokolewa; kila mmoja atakayeonekana ameandikwa katika kitabu kile.
Ule ushuhuda wa Yesu uko wazi katika mazungumzo ya Yesu na Yohana kwamba ni Roho ya Unabii (Uf.19:10 cf.
Ufunuo 19:10X
10 Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.
Uf.22:9).
Ufunuo 22:9X
9 Naye akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako, na wa ndugu zako manabii, na wa wale wayashikao maneno ya kitabu hiki. Msujudie Mungu.
Kukosekana kwa Roho ya Unabii kunafanya sheria ya Mungu idharauliwe (Omb. 2:9).
Maombolezo 2:9X
9 Malango yake yamezama katika nchi; Ameyaharibu makomeo yake na kuyavunja; Mfalme wake na wakuu wake wanakaa Kati ya mataifa wasio na sheria; Naam, manabii wake hawapati maono Yatokayo kwa Bwana.
Mungu alitoa karama ya unabii kuongoza watu wake waliotoka Misri (Mdo. 7:38,
Matendo 7:38X
38 Yeye ndiye aliyekuwa katika kanisa jangwani pamoja na yule malaika aliyesema naye katika mlima wa Sinai, tena pamoja na baba zetu; ndiye aliyepokea maneno ya uzima atupe sisi.
Hos.12:13).
Hosea 12:13X
13 Na kwa nabii Bwana alimtoa Israeli katika Misri, Na kwa mkono wa nabii alihifadhiwa.
Watu wa Mungu kuihama dunia kutakamilisha unabii wa “Katika siku hiyo Bwana atapeleka mkono wake mara ya pili ili ajipatie watu wake watakaosalia” (Isa.11:11)
Isaya 11:11X
11 Na itakuwa katika siku hiyo, Bwana atapeleka mkono wake mara ya pili, ili ajipatie watu wake watakaosalia, kutoka Ashuru, na kutoka Misri, na kutoka Pathrosi, na kutoka Kushi, na kutoka Elamu, na kutoka Shinari, na kutoka Hamathi, na kutoka visiwa vya bahari.

Kupima Karama ya Unabii

Kwa kuwa watakuja manabii wa uwongo na wito wa Paulo kwamba “msitweze unabii, pimeni mambo yote, chagueni lililo jema (1Thes.5: 20-22 cf.

1 Wathesalonike 5:20-22 X
20 msitweze unabii; 21 jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema; 22 jitengeni na ubaya wa kila namna.
cf. 1Yoh. 4:1),
1 Yohana 4:1X
1 Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani.
ni vema kuwa na vigezo vya kuwapima manabii, tujue kwamba wametumwa na Mungu. Vigezo vifuatavyo vinafaa sana: -

  • Je ujumbe unakubaliana na Biblia? “Na waende kwa sheria na ushuhuda, kama hawasemi sawasawa na neno hili ni kwa sababu hao hakuna asubuhi”(Isa.8:20 cf.
    Isaya 8:20
    20 Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao hapana asubuhi.
    Kumb.13:1-4)
    K. Torati 13:1-4X
    1 Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, 2 ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; 3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote. 4 Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye.
    Roho za manabii hutii manabii (1Kor. 14:32)
    1 Wakorintho 14:32X
    32 Na roho za manabii huwatii manabii.
    na pia kwa Mungu hakuna kugeuka geuka (Yak.1:17).
    Yakobo 1:17X
    17 Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka.
  • Je atabiricho kinatimia? Tutajuache kwamba huyu ametumwa na Bwana, ni kwamba anachosema ni lazima kitimie (Kumb.18:21, 22 cf.
    K. Torati 18:21,22X
    21 Nawe ukisema moyoni mwako, Tutajuaje neno asilolinena Bwana? 22 Atakaponena nabii kwa jina la Bwana, lisifuate jambo lile wala kutimia, hilo ndilo neno asilolinena Bwana; kwa kujikinai amelinena huyo nabii, usimwogope.
    Jer. 28: 9).
    Jeremia 28:9X
    9 Nabii atabiriye habari za amani, neno la nabii yule litakapotokea, ndipo nabii yule atakapojulikana, kuwa Bwana amemtuma kweli kweli.
    Hata hivyo ni vema kuzingatia unabii wenye masharti (Jer. 18:7-9).
    Jeremia 18:7-9X
    7 Wakati wo wote nitakapotoa habari za taifa, na habari za ufalme, kuung'oa, na kuuvunja, na kuuangamiza; 8 ikiwa taifa lile nililolitaja litageuka, na kuacha maovu yake nitaghairi, nisitende mabaya yale niliyoazimia kuwatenda. 9 Na wakati wo wote nitakapotoa habari za taifa, na habari za ufalme, kuujenga na kuupanda,
  • Je, kufanyika mwili kwa Kristo kunaheshimiwa? Akikiri Yesu amekuja katika mwili atakubalika, akikataa basi hakubaliki (1Yoh. 4:1-3).
    1 Yohana 4:1-3X
    1 Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. 2 Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. 3 Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.
  • Je, nabii ana matunda mema au mabaya? Kwa kuwa unabii unatoka kwa Mungu (2Pet 1:21)
    2 Petro 1:21X
    21 Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
    lazima matunda yake yawe mema. “Mtawatambua kwa matunda yao” (Mt. 7:16, 18-20).
    Mathayo 7:16, 18-20X
    16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? 20 Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.
    Eliya alikuwa na hali ya kibiunadamu (Yak.5:17)
    Yakobo 5:17X
    17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.
    hata hivyo, maisha yake hayakuwa ya kimwili bali yalijawa na tunda la roho (Gal. 5:19-22).
    (Wagalatia 5:19-22X
    19 Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. 22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
    Pili, matokeo yake kazi ya nabii daima ni kulisaidia kanisa (Efe.4:12-16)
    Waefeso 4:12-16
    12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; 13 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo; 14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu. 15 Lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo. 16 Katika yeye mwili wote ukiungamanishwa na kushikanishwa kwa msaada wa kila kiungo, kwa kadiri ya utendaji wa kila sehemu moja moja, huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo.

Roho ya Unabii katika Kanisa la Waadventista Wasabato

Karama ya unabii ilijidhihirisha katika huduma ya Mama Ellen G. White, mojawapo ya waanzilishi wa Kanisa.

Tangu mwaka 1844 alipokuwa na miaka 17 hadi mwaka aliofikwa na mauti 1915, alipata maono zaidi ya 2,000. Alifanya kazi Marekani, Ulaya na Australia akishauri, akifungua kazi, akihubiri na kuandika. Kwa kumpima kwa vigezo tulivyobainisha, anatosheleza kabisa.

  1. Kukubaliana na Biblia: Kazi yake ya uandishi imenukuu aya maelfu za Biblia, mara nyingi yakifafanuliwa. Uchunguzi makini umedhihirisha kwamba maandiko yake yanalingana, ni sahihi na yanapatana kabisa na Biblia.
  2. Usahihi wa Utabiri: Ellen alitabiri mengi na mengine yanasubiri kutimizwa. Hata hivyo, yaliyotimia ni (1) Kuinuka kwa umizimu – mwaka 1850 wakati umizimu unaanza alionya kwamba ni udanganyifu utakaoendelea hadi siku za mwisho. (2) Ushirikiano wa karibu baina ya Ukatoliki na Uprotestanti (3) Kazi ya kuchapa vitabu, kwamba mwanzo wake ni mdogo lakini hatimaye utafaulu.
  3. Kumkiri Yesu katika mwili: Katika kitabu chake cha Tumaini la Vizazi Vyote (Desire of Ages) Mama White amekiri kwamba Yesu amekuja katika mwili. Pia kwenye kitabu cha Njia Salama (Steps to Christ) anamkiri Yesu.
  4. Mvuto wa Kazi yake: Zaidi ya karne na nusu imepita tangu afariki, lakini maoni haya yanawakilisha vema mguso wake: Ingawa hakuwa ofisa wa kanisa wala hakupokea mshahara hadi mume wake alipofariki, kando ya Biblia, huduma yake ndiyo imeunda sura ya Kanisa la Waadventista wa Sabato.” Richard Hammill, Karama za Roho katika Kanisa Leo, Ministry Julai 1982.

Roho ya Unabii na Biblia

Maandiko ya Ellen White siyo badala ya Maandiko Matakatifu. Haiwezekani kuwekwa kwenye ngazi sawa. Maandiko Matakatifu husimama peke yake, kiwango pekee cha kupima mafundisho yote pamoja na maandishi ya Ellen White.

  1. Biblia kipimo pekee: Waadventista Wasabato huamini katika kanuni ya Sola Scriptura kwamba Biblia na Biblia peke yake ndiyo mtafsiri wake, na msingi wa mafundisho yote. Kanisa halikupokea mafundisho yake kutoka kwa Ellen White ila kutoka kwenye Biblia. Huduma yake ilisaidia kuelewa Biblia na kuthibitisha hitimisho lililofikiwa kwa kusoma Biblia.
  2. Kuongoza Kwenye Biblia: Yeye mwenyewe aliona kazi yake kuwa ni kuongoza watu kurudi kwenye Biblia, kwa kuwa watu walikuwa wameacha kuifuata.
  3. Kuongoza kuelewa Biblia: Ellen White aliona kuwa mafundisho yake yanasaidia mtu kuelewa vema Biblia. Shuhuda zilizotolewa siyo nuru mpya, bali hukazia nuru iliyokwisha kutolewa yaani Biblia.
  4. Kuongoza kutumia Kanuni za Biblia: Unabii wa Ufunuo utadhihirika pale ambako kila moja atapima na kuchukua kilicho chema. Twaweza kupata au kupoteza kulingana na jinsi tunavyochunguza Maandiko.

Maisha na Huduma ya Ellen White

(Dondoo kutoka Church Heritage)
  1. Alizaliwa Novemba 26, 1827 shambani Gorham, Maine, kama maili 12 kutoka Portland. Akiwa na pacha mwenzake, alikuwa mdogo kuliko wote katika familia yenye watoto wanane. Alikuwa mtoto mwenye furaha akipenda sana mambo ya imani.
  2. Maisha yake yalibadilika siku moja wakati akiwa anavuka Park alipopigwa jiwe na msichana mwingine. Pua yake ilivunjika na uso wake uliharibika kwa muda. Alizimia wiki tatu na mshtuko ulimfanya asiweze kufanya chochote kwa wakati mrefu. Kusoma kwake kulikoma kwa kuwa afya yake haikuruhusu.
  3. Mwaka 1840 hadi mwaka 1844 Ellen na familia yao walisikiliza mahubiri ya William Miller, juu ya ujio wa Yesu ulivyo karibu. Walikubaliana na mahubiri na hawakuhama kutoka kwenye kanisa lao la Methodist. Hata hivyo haikuwa rahisi. Katika mkutano wa kambi mojawapo, alijitoa na ndipo roho yake ilipotulia. Tangu wakati huo alianza mahusiano mapya na Bwana wake.
  4. Familia yake ilikubali Kilio cha Usiku wa Manane na kuacha makanisa yaliyoasi – yaani yaliyokataa ujumbe wa Yesu kurejea mara ya pili. Pamoja na kwamba Yesu hakurudi kama walivyotarajia, hawakukata tamaa kuacha imani yao.
  5. Maono yake ya kwanza yalikuja muda mfupi baada ya mategemeo yao ya Yesu kurejea kutokutimizwa. Akiwa na umri mdogo (miaka 17), uwezo wake mdogo kuongea, afya yake iliyozorota, na kipindi kigumu alichokabiliana nacho, alimwomba Mungu amwepushe na jukumu la kuwa mjumbe wake. Hata hivyo wito wake haukubadilishwa, na hivyo alikubali kufanya kile ambacho Mungu alimwamuru.
  6. Apili Mwaka 1847 alipewa njozi ya Sabato. Aliona Hekalu mbinguni Yesu akifungua pazia. Kwenye Patakatifu pa Patakatifu, aliona Amri Kumi za Mungu na mng’ao wa mwanga ukimulika amri ya nne, ambayo ni Sabato. Akajulishwa kwamba kama Sabato ingeendelea kutunzwa kwa uaminifu na wanadamu, asingekuwako asiyeamini Mungu, wenye mashaka na ulimwengu usingeingia kwenye ibada ya sanamu. Njozi hii, ilifungua mlango wa kuhubiri ujumbe wa Malaika wa Tatu kwa nguvu. Waumini walioona umuhimu wa Patakatifu, Sabato na Ujio wa Yesu mara ya pili, walikuja kuwa waanzilishi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato. (Life Sketches pp. 95)
  7. Kwa miaka 70 iliyofuata, jukumu lake lilikuwa kupokea mashauri kutoka kwa Mungu naye aliyatoa kwa watu wake. Alizungumza katika mikutano mingi na aliandika vitabu vipatavyo 40 ambavyo vilikuja kujulikana kama Roho ya Unabii, akachangia pia kuchapisha makala nyingi katika machapisho ya kanisa la Waadventista wa Sabato. Kitabu kinachopendwa zaidi ni habari za maisha ya Yesu – Tumaini la Vizazi Vyote. Alisafiri kuzunguka sehemu nyingi za Amerika Kaskazini, Ulaya, Australia na New Zealand, akifungua kazi katika maeneo mapya. Alikuwa muhimu katika kufungua chuo cha Avondale kilichoko Australia.
  8. Ellen White alipokea ujumbe kwa njia ya maono. Katika maono, uko ushahidi kwamba aliongozwa na Mungu. Aliangalia vitu vilivyo mbali, kuhema kwake kulikoma lakini hakubadilika rangi wala moyo wake haukukoma kudunda. Shuhuda za waliomwona, pamoja na madaktari, walishuhudia kwamba utaratibu wote haukuwa wa kidunia. Kuna wakati alibeba Biblia kubwa ya paundi 18 kwa nusu saa pasipo kuyumba wala kuidondosha.
  9. Baadhi ya vitabu alivyoandika ni Shuhuda kwa Kanisa (1855-4909), Early Writings (1882), The Great Controversy (1888), Patriarchs and Prophets (1890), Gospel Workers (1892), Steps to Christ (1892), Thoughts from the Mount of Blessings (1896), Christ’s Object Lessons (1900), Education (1903), The Ministry of Healing (1905), The Acts of Apostles (1911), Counsels to Parents, Teachers and Students (1913), Prophets and Kings (1916).
  10. 10. Ellen White alilala usingizi wa mauti nyumbani kwake Elmshaven Julai 16, 1915 akazikwa alikozikwa mume wake na watoto wake Battle Creek.

×0001020304050607080910111213141516171819202122232425262728