Mafundisho Makuu ya Biblia
Mafundisho ya Biblia ni seti ya mada za msingi katika Biblia, zinazotusaidia kuelewa kile Biblia inachofundisha katika ujumla wake. Mada hizi za Biblia husaidia kueleza ukweli wa msingi kuhusu Mungu, mwanadamu, na wokovu kwa namna iliyopangiliwa vizuri. Mafundisho haya yanachukuliwa kuwa ya muhimu sana katika Imani ya Kikristo kwa kuwa yanatoa mfumo wa kuielewa tabia ya Mungu, uhusiano wetu na Yeye, na kuonesha njia ya uzima wa milele. Mafundisho yote ya Biblia yanaweza kuainishwa katika mada au mafundisho au imani 28 za msingi, ambazo zimegawanyika katika mafundisho makuu sita ya Biblia ambayo ni: Mungu, Mwanadamu, Wokovu, Kanisa, Maisha ya Kikristo, na Matukio ya Siku za Mwisho
Fundisho Kuhusu Mungu
Mafundisho haya yanafundisha kuhusu namna Mungu anavyowasiliana na mwanadamu na kumuonesha asili Yake, sifa Zake, na matendo yake makuu kama Muumbaji na Mkombozi. Fundisho hili hueleza namna Mungu anavyotaka tufahamu jinsi alivyo mkuu na kuitambua mamlaka Yake kama mamlaka ya juu kabisa. Imani za Msingi katika mafundisho haya ni:
Fundisho Kuhusu Mwanadamu
Fundisho hili hufafanua chimbuko la mwanadamu, likieleza kuanza kwa dhambi duniani na madhara yake. Linaonesha kusudi la ubinadamu na hitaji la ukombozi. Linafafanua namna Biblia inavyoeleza juu ya utambulisho wa binadamu na kuweka msingi wa wajibu wa kimaadili. Imani za Msingi ndani ya Fundisho hili ni pamoja na:
Fundisho Kuhusu Wokovu
Fundisho hili hueleza mchakato wa ukombozi ulivyo likifafanua umuhimu wa kifo na ufufuo wa Yesu Kristo. Hapa ndipo tunapojifunza sehemu ya neema na imani katika kuutafuta uzima wa milele. Fundisho hili hufafanua jinsi Mungu anavyowapatanisha wanadamu na Yeye Mwenyewe. Imani za msingi katika fundisho hili ni:
Fundisho Kuhusu Kanisa
Fundisho hili linafafanua na kueleza namna ya kulitambua Kanisa la Mungu, na utume wa Kanisa. Hapa tunajifunza namna Biblia inavyofafanua suala la la ibada, na kuelekeza namna Mungu anavyoliagiza Kanisa lake kuisambaza Injili. Fundisho hili linawasaidia waumini kuelewa wajibu wao katika mpango wa Mungu wa Wokovu. Imani za msingi katika mafundisho haya ni:
Fundisho Kuhusu Maisha ya Kikristo
Fundisho hili huwawaongoza watu kuishi huki wakiwa na utii kwa Mungu. Husisitiza utakatifu, upendo, na tabia bora inayompendeza Mungu. Ni fundisho linaloonyesha jinsi ya kutumia kanuni za kibiblia katika maisha ya kila siku. Imani za msingi katika mafundisho haya ni:
Fundisho Kuhusu Mambo ya Mwisho
Fundisho hili linahusu mambo ya nyakati za mwisho, kurudi kwa Kristo, na hukumu ya mwisho. Fundisho hili huwahimiza na kueleza namna watu wanavyoweza kubaki wakiwa waaminifu huku wakitarajia uzima wa milele. Imani za msingi zinazozungumzia mambo ya mwisho ni:
